Saturday, February 2, 2019

IMAGE OF RAIN WATER HARVESTING

RAINWATER HARVESTING

What Is Rain Water Harvesting?





So what is rainwater harvesting? It is a technique or strategy for the collection of rainwater and storing it in the right way for future use. The water can be collected from various surfaces and platforms and stored for later use. In most cases, the water is usually collected from rooftops and other hard surfaces. Rainwater harvesting is considered a very reliable way to conserve water.

This technique has been around for a very long time, practiced in the ancient times. Over the past years, this ancient method of water storage has grown quite popular. It plays a vital role in reducing the use of potable water and increase reliability on rainwater.

Advantages of Rainwater Harvesting

 In both urban and rural setting, harvesting can be done by the use of infrastructure. One of the simplest ways of storing water from the collection is storage tanks. In most cases, the harvested water is usually redirected to storage tanks, cistern or reservoirs. The water is usually stored for later use. The roof of buildings is the best way to harvest rainwater. There are numerous advantages in doing so.
1. Easy to Maintain
 The use of rainwater harvesting system provides ideal merits to any community. First and foremost, the collection offers better and efficient utilisation of energy resource. It is important because potable water is usually not renewable, thus reducing wastage. The systems used for water collection is based on simple techniques that are very easy to maintain. The overall expenses used in setting up harvesting methods are much cheaper compared to other purifying or pumping means. Also, its maintenance is feasible on the economic front as it does not require deep pockets.
2. Reducing Water Bills
Water that has been stored from harvesting water can be used for several non-drinking purposes. It will immediately reduce one’s utility bills. It is ideal for both residential and commercial properties.
3. Suitable for Irrigation
Harvesting allows the collection of large amounts of water. Most rooftops provide the necessary platform for collecting water. Rainwater is usually free from harmful chemicals, which makes it ideal for irrigation purposes.
4. Reduce demand on Ground Water
Another important advantage is that it reduces the demand for potable water. It is important especially in areas with low water levels.
These are some of the significant advantages of har









Techniques of Rainwater Harvesting


The collection of rainwater can be done in various methods depending on a few factors. A few common methods include the following:
1. Rain barrels
 It is the easiest and affordable method of rainwater harvesting, especially at home. It is where barrels or water tanks installed below the downspouts of the rooftops guttering system. The water is then funnelled/directed into the tanks. The tank can be connected to provide backup water to your current plumbing system, or it can be attached to a pipe for drip irrigation. The use of barrels or tanks is ideal since it can store significant amounts of water.
2. Dry System
It is similar to the barrel’s system, but with the dry system, a larger storage container is used. The container is usually a few meters away from the property. The gutter is redesigned so that water is diverted to the large storage tank. It is a quick and cheap method to implement but has significant rewards.
3. Wet System
It is a technique that is entirely different from the dry system. Here, the collection pipes will always have water in them. It is because they will be situated underground. In the wet system, many collection pipes are connected to the downspouts of a building and diverted into a storage tank, which is also underground. The pipes need to be secure and well maintained to ensure there is no leakage into the soil.
4. Green Roof
This method of harvesting does not need the use of storage tanks. Instead of storing the water in a reservoir, the water is channelled straight to the garden. The process will require installing a drainage system on a building’s roof straight to the backyard. It is a very low maintenance method.
These are few of the standard rainwater harvesting methods, which are mainly done in many households.

How Rainwater Harvesting Solves Water Shortage?

Harvesting and collection of rainwater is a proper way that can be used to address the problem of the water crisis in various parts of the world. This simple water conservation method can be used to put forward a remarkable solution in areas where there is enough rainfall but not enough supply of groundwater.
Bangalore is an excellent example where rainwater harvesting can become very beneficial. Bangalore is an area with a very high population and an area that also has to deal with water shortages. With these in mind, practising water conservation methods such as rainwater harvesting is an ideal way to ensure an increased supply of water.
Bangalore experiences quite an immense amount of rainfall almost throughout the year. Hence, rainwater harvesting will play a huge role in providing additional sources of water. During the dry season, people will be able to have water sources if they have implemented the necessary kind of harvesting techniques. With increased demand for water, rainwater collection can be able to meet the requirements.
When builders and architects are designing a new home or building, it is important that they think of implementing rainwater harvesting methods. It will be able to reduce reliability on other natural resources for groundwater. In the long run, there will be energy savings, water savings, and resource savings.
Click the link to view image of rainwater harvesting   https://www.google.com/search?q=rain+water+harvesting&source=lnms&tbm=isch&sa=X&ved=0ahUKEwjD4M73lZ3gAhUnRxUIHXBPD3wQ_AUIDigB&biw=1024&bih=657

Saturday, January 26, 2019

JINSI YA KUPATA UTAJIRI
Imeandaliwa na
Hassan Issa Khamis
hansb2269@gmail.com

Kila mtu anahitaji kuwa tajiri na matajiri wanahitaji kuendelea kuwa matajiri katika maisha yao, lakini ni watu wachache sana waonajua wafanye nini ili waweze kuwa matajiri. Kuwa tajiri huchukua mchanganyiko wa mambo matatu,
·         Bahati,
·         Ujuzi na
·         Uvumilivu. 
Vile vile utahitajika kujiweka kwenye mambo yanayoopelekea kupata faida, kutumia fedha unazopata kwa busara kwa kuziwekeza, kuzihifadhi, na kupunguza gharama zako za maisha. Kupata utajiri si rahisi, lakini ukiwa na uvumilivu na ujuzi wa kufanya maamuzi, ni dhahiri inawezekana.
NJIA YAKWANZA: UWEKEZAJI
Wekeza fedha zako kwenye hifadhi itakupa faida kwa kila mwaka kwenye uwekezaji (ROI). Kwa mfano, ukiwekeza milioni mbili katika taasisi yenye riba 7%, utapata faida ya 140,000. Maelezo kuhusu soko la hisa bonyeza linki hapo chini.
2.      Usiekeze biashara ya muda mrefu. 
Watu wengine wanajihusisha katika biashara yenye faida ya haraka, ambapo mwisho wa siku biashara ushindwa kuendelea, kuishia kudaiwa fedha na taasisi za fedha au watu pamoja na kuweka rehani mali zao. Watu wanapenda kufanya biashara ya muda mfupi kwa kuuza haraka na kupata faida kwa haraka. Biashara ya muda mfupi au yenye faida ya haraka ni  kama kamari.  Badala yake, jifunze kuwekeza kwa muda mrefu. Chagua biashara nzuri, weka msingi thabiti katika hiyo biashara. Hepuka marafiki wanaokuambia biashara Fulani inalipa alafu wao hawaifanyi, fanya biashara ambayo wewe unaipenda.
3.      Nunua hisa.
Watu wengi hawana elimu ya kutosha katika soko la hisa. Ukinunua hiza katika makampuni au taasisi, hisa zako zitakua na kuleta faida baadae. Kwa mfano Airtel wamekubali kuuza hisa zake nchini ni moja ya fursa ya kuchangamkia. Kuapata taarifa zaidi tembelea tofutti ya soko la hiza Tanzania.

Takwimu zinaonesha  kwamba watu wachache wanahifadhi pesa za kutosha kwa ajili ya kustaafu au maisha ya uzeeni. Ila wengine wanahisi kuwa hawawezi kamwe kustaafu au kuzeeka.kipindi ambacho bado una nguvu za kutosha wekeza katika kuandaa maisha yako ya baadae ili usije ukawa mzee masikini. Unaweza kufanya yafuatayo:-
i)                    Kusomesha watoto
ii)                  Kujenga nyumba imara
iii)                Kununua maeneo yanauzwa kwa bei nafuu.
iv)                Kuhifadhi pesa benki.
v)                  Kufungua biashara endelevu. nk
Mali isiyohamishika kama nyumba ya kupangisha au kiwanja katika eneo linalo kuwa kwa kasi ni njia nzuri ya kujenga utajiri.  Watu wengi, hata hivyo, wamefanya vizuri sana katika uwekezaji katika mali isiyohamishika. 
6.      Wekeza muda wako. 
Kwa mfano, unapokuwa na  na muda wa bure, tenga saa chache kufanya kitu. Lakini ukiamua kuwa tajiri fanya kazi hadi saa 15 kwa siku.  
Kutumia 15,000,000 kwenye gari wakati mwingine ni upotezaji wa fedha, kwa sababu inawezekana baada tu yakuinunua  haitakuwa na thamani ya hela uliyoinunulia. Unapoiendesha gari mpya kwenye barabara inapungua dhamani kwa 20% -25% na inaendelea kufanya hivyo kila siku. 
8.      Usitumie pesa kwenye mambo ya kijinga. 
Usikubali kutumia fedha zako ngumu kwenye mambo ya kijinga. Jiepushe na michezo ya kubahatisha mfano. 
-       Casino na tiketi za bahati nasibu. Kwani wachache hupata bahati ya kushinda lakini waliowengi hupoteza.
-       Uvutaji sigara . Wanaovuta sigara wanaweza kutazama pesa zao tu kwenye moshi wa sigara.
-       Huwanywaji wa pombe uliopitiliza

NJIA YA PILI: TAJIRIKA KUPITIA KUFANYA KAZI
1.      Jiongeze  kitaaluma.

 Kupitia kujiongeza kitaaluma kutakufanya kupanda kuongeza ufanisi katika ufanyaji wako wa kazi. Hivyo unaweza kuongezewa kiwango cha mshahara pamoja na kupanda cheo. 
2.      Chagua taaluma sahihi . 
Kama haujasomea kazi au unataka kujiongeza kitaaluma angalia tafiti za mishahara ambazo zinaonyesha mapato ya wastani ya kila mwaka kwa fani maalum. Vigezo  vyako vya kupata utajiri vitapungua ikiwa utasomea kazi yenye kipato kidogo. Hapa ni baadhi ya ajira zinazolipa zaidi. Kwa mfano taaluma za Udaktari, Uhandisi wa petrol na gesi, sheria, utunza fedha, siasa, Tehama n.k  wana nafasi kubwa ya kuwapata fedha nyingi, wanaweza kuingiza zaidi ya Tsh 30,000,000 kwa mwaka.
3.      Chagua eneo sahihi . 
Nenda kafanye kazi sehemu/eneo zuri lenye fursa.  Kuna fursa nyingi zaidi katika miji mikubwa kuliko maeneo ya vijijini, vijijini kunaweza kuwa sehemu ya kuanzia, ukitaka kufanya kazi pamoja na biashara, nenda kafanye kazi katika miji yenye watu wengi.
Omba kazi maeneo mengi na ujishughulishe na mahojiano mengi. Unapopata kazi, ifanye kwa juhudi  ilikupata uzoefu na kupanda vyeo. Kazi ambazo hazina nafasi za kupanda hazimpi mtu motisha ya kufanya kazi na umkosesha kipato.

5.      Badilisha ajira na mwajiri . 
Mara tu upatapo uzoefu kwenye fan/kazi yako, fikiria kupata kazi mpya au majukmu mapya. Hii itakufanya kubadilisha mazingira yako kazi, unaweza kuongeza kipato chako na uzoefu wa tamaduni tofauti za ufanyaji kazi. Usiogope kufanya hivyo mara kadhaa. Ikiwa wewe ni mfanyakazi wa thamani, pia inawezekana kuwa kampuni/taasisi yako ya sasa inaweza kukupa faida (kukuongezea malipo) au faida nyingine yoyote  ikiwa wanajua unataka kuondoka.
NJIA YA TATU: KUPUNGUZA GHARAMA ZA MAISHA
1.      Jifunze kuhifadhi chakula na mahitaji mengine . 
Ukiwa na ziada ya chakula ndani itakusaidia kuweka akiba kutoka katika vipato vyako. Kuliko kila siku unanunua mahaji. Nunua jokovu hifadhi chakula kinacho baki hii ni hazina ya siku nyingine.
Umeme, gesi, na huduma zingine zinaweza kuathiri bajeti yako ya kila mwezi ikiwa vitatumika vibaya. Mfano taa zote ndani ya nyumba kuwashwa kwa wakati mmoja alafu baadhi ya maeneo hamna mtu, kupika chakula kingi na kulazimisha kukimaliza, kuchemsha maji ya kuoga baadala ya kufanya mazoezi kisha ukaoga maji ya kawaida nk. Kwahiyo shusha bili zako na utafakari kabla ya kulipia bili mbali mbali.
NJIA YA NNE: KUOKOA FEDHA
1.      Jilipe kwanza . 
Hii inamaanisha kabla ya kwenda kutumia mshahara wako au kipato chako weka pesa katika akiba yako, unaweza kuweka kwenye kibubu au akaunti au kwenye mtandao wa simu. Fanya hivi kila wakati unapolipwa mshahara au kupata kipato chochote na uhakikishe akiba yako inakua.
2.      Panga bajeti yako
Tengeneza  bajeti ya kila mwezi ambayo inhusu gharama zako zote za msingi na acha hela kidogo kando ya kustarehe/kujiburudisha/dharura. Zingatia bajeti yako ilikuokoa fedha angalau kila mwezi nah ii ni mmoja ya  jitihada  za kuwa tajiri.
3.      Punguza gharama katika usafiri na makazi . 
Hivi, ungependa kuwa na ghorofa badala ya nyumba ya kawaida ? Je ni lazima kununua usafiri badala ya kutumia usafiri wa kawaida? Kuna haja ya kujenga nyumba yako ikiwa gharama za kupanga nyumba ziko chini? Je! Unaweza kununua gari ambalo limetumika badala ya mpya na kuitumia kwa upole? Haya ni maswali ambayo unatakiwa kujiuliza ili  kuhifadhi tani ya fedha kila mwezi.
4.      Kata gharama .
 Angalia njia ambazo hutumia fedha nyingi kisha tafakari. Kwa mfano, nunua vitu siku za minada ambapo gharama zinakuwa chini. Pia nunua vitu original ili vitumike kwa muda mrefu badala ya kila siku unanunua kitu ambacho ulishawahi kukinunua.
5.      Achana  mikopo isiyokuwa na ulazima . 
Lipa bei  kamili kwa wakati ili kukwepa riba isiyo na ulazima. Kwa mfano kukopa vocha ya shilingi 600 kisha unalipa 700 ukijumlisha na riba ya shilingi 100.
Bottom of Form


Monday, January 21, 2019

Sunday, January 20, 2019

Mwezi mkubwa mwekundu kuonekana duniani


Mwezi mkubwa mwekundu
Watu kote duniani wanatarajiwa kuona kupatwa kwa mwezi utakaobadilika na kuwa mwekundu .
Wakati wa kupatwa kwa mwez,i dunia hutoa kivuli chekundu.
Kupatwa huko kwa mwezi kutaonekana kutoka kaskazini na Kusini mwa Marekani pamoja na maeneo ya magharibi mwa Ulaya ikiwemo Uingereza na kaskazini mwa Afrika

Kupatwa kwa mwezi ni nini?

Tukio hili hujiri wakati dunia inapopita katikati ya Jua na mwezi.
Katika hali hii, jua huwa nyuma ya dunia huku mwezi ukizunguka katika kivuli cha dunia.

Je mwezi mwekundu ni upi?

Maelzo ya mwezi mwekundu
Presentational white space

Je mwezi huo utakuwa mwekundu?

Ndio. Baadhi ya watangazaji huuita "super blood wolf moon".
Jina "super" linatokana na ukweli kwamba mwezi huo utakuwa karibu sana na dunia ambapo utaonekana kuwa mkubwa angani zaidi ya kawaida.
Nalo Jina "wolf" linatokana na majina yanayopewa miezi mikubwa mwezi Januari "wolf moons".
Walter freeman , naibu profesa katika chuo kikuu cha Syracuse University mjini New York state, alisema: "mwanga mdogo wa jua hutolewa na dunia na kufika katika mwezi, ukijipinda kando kando ya dunia.
Kiwango hiki cha rangi nyekundu huangazia mwezi vya kutosha kwa binadamu kuweza kuona.

Wapi na lini nitauona mnwezi huo?

Kupatwa kwa mwezi kutaanza mwendo wa 02:35 GMT siku ya Monday na kukamilika katika saa 07:49 GMT, lakini kipindi ambacho mwezi wote utakuwa mwekundu kitakuwa mwendo wa 05:12 GMT.
Nchini Uingereza mwezi utakuwa juu ya upeo wa macho katika kipindi chote cha kupatwa kwa mwezi ijapokuwa kusini mashariki mwa Uingereza, jua litaonekana kupaa huku luna hiyo ikikamilika.
Kupatwa huko kutaonekana kaskazini magharibi mwa Ufaransa, kaskani magharibi mwa Uhispania, Ureno, na eneo dogo la Afrika magharibi, karibu eneo lote la kaskazni na Amerika Kusini, mashariki mwa Pacific pamoja na kilele cha Ksakzini mashairiki mwa Urusi.

Je ni salama kuutazama?

Huku matukio ya kupatwa kwa mwezi yakitajwa kuwa hatari kutazama moja kwa moja, mwangaza wa kupatwa kwa mwezi ni mdogo hivyobasi ni salama kutazama bila kutumia vifaa vyovyote.

Je ina muhimu gani?

Tukio hilo ni la mwisho kwa watazamaji wa anga nchini Uingereza kuona kupatwa kwa mwezi kwa kipindi cha muda mrefu hadi 2029- hali ya hewa itakaporuhusu.

Thursday, July 21, 2016

KUELEKEA MKUTANO WA CCM KINANA AONGEA

Kinana atoa Masharti Endapo Rais Magufuli Atamhitaji Aendelee Kuwa Katibu Mkuu wa CCM

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana ametoa neno endapo Rais John Magufuli atamhitaji kuendelea na wadhifa huo, huku akibainisha kuwa amekutana na changamoto nyingi katika nafasi hiyo kiasi kwamba wakati mwingine alikata tamaa.

Mwanasiasa huyo maarufu ndani ya CCM na nchini, anatarajiwa kuhitimisha uongozi wake wiki hii wakati Mwenyekiti mpya wa CCM Taifa, Rais John Magufuli atakapokabidhiwa uenyekiti huo na kuunda Sekretarieti yake mpya ambayo haijulikani kama itaongozwa tena na Kanali huyo wa zamani wa Jeshi.

Akizungumza jana na waandishi wa habari baada ya kukagua Ukumbi wa Mkutano Maalumu wa CCM utakaofanyika keshokutwa Jumamosi, Kinana ambaye amekuwa katika nafasi hiyo kwa miaka mitatu na nusu, alisema aliombwa katika nafasi hiyo baada ya kuwa aliamua kustaafu, lakini akakumbana na changamoto mbalimbali.

CCM kuwa mbali na wananchi 
Alisema kuna wakati aliona kama vile chama kiliacha kwenda kwa wananchi na kwamba hakikuwa karibu sana nao.

“Ninyi ni mashahidi, ikabidi kubuni utaratibu mzuri wa kwenda kwa wananchi ili chama kiwe karibu na wananchi, kiwasikilize na kuwa sauti ya wananchi kifuatilie matatizo yao kisimamie utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi,” alisema Kinana na kuongeza kuwa katika kufanya hivyo amekuwa akiwasiliana na Rais na Waziri Mkuu kwa ajili ya matatizo kutatuliwa.

“Changamoto ya pili ya kuimarisha umoja na mshikamano ndani ya chama, hapo nyuma kulikuwa na misukosuko kidogo ya umoja na mshikamano, kushutumiana na kulaumiana,” alisema na kuongeza kuwa kazi nyingine aliyofanya ni kuimarisha umoja ndani ya chama, kushirikiana na viongozi wenzake kuhakikisha chama kinajitahidi kwa kadri ya uwezo wake kurejea katika misingi yake ya awali katika maeneo ya uadilifu, uwajibikaji na utendaji kazi kwa ufanisi.

Azuiwa ziarani
Kinana alisema amekwenda wilaya zote, majimbo, mikoa na nusu ya kata za nchi na amesafiri zaidi ya kilometa 192,000, kufanya mikutano zaidi ya 3,700 ya aina mbalimbali ya ndani na nje na haikuwa kazi rahisi

 “Changamoto nilizokutana nazo ambazo lazima nikiri ni pale nilipotaka wakati mwingine kufanya ziara kwenye maeneo fulani fulani niliambiwa ni hatarishi siwezi kwenda kwa hiyo ilibidi nibishane na viongozi na watendaji wakuu wa serikali…nikasema hapana nimeamua kwenda lazima niende,” alisema Kinana.

Katibu huyo akitoa mfano alisema kuna wakati aliamua kutoka kwa boti kutoka Nyamisati wilayani Rufiji kwenda Mafia, viongozi wa Mkoa wa Pwani walifikiri si njia salama ya kusafiri na kumpelekea ujumbe asisafiri kwa boti, bali asafiri kwa ndege, lakini alisema hapana ataondoka kwa boti.

“Walichofanya wakakaa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na wakaniandikia barua rasmi kwamba tunakushauri usisafiri kwa boti safiri kwa ndege kwa maana nyingine walikuwa wanajivua lawama kwa yatakayotokea, lakini vile vile kunitisha kidogo kwamba si salama zaidi nikawasisitiza hapana,” alieleza Kinana.

Ashitakiwa kwa JK
“Baadaye Rais mstaafu Kikwete alikuwa Msoga, viongozi wa Mkoa wa Pwani wakaenda kumwambia tumezungumza na Katibu Mkuu wako naona hasikii tumemuandikia barua ya kumuomba asisafiri na boti hasikii, Rais akaandika meseji ndefu sana…nikamjibu rais nakuheshimu mamlaka yako ni makubwa si vizuri nikakukatalia, lakini niruhusu nikukatalie kwa sababu hata wananchi wanaosafiri kwenye boti hii wanahatarisha maisha yao, ni vizuri na mimi nikahatarisha maisha yangu hata kidogo… akaniambia nimekuelewa endelea,” alibainisha.

Alisema zipo changamoto nyingi sana nyingine, kwa mfano Mbambabay kwenda Kyela, mkuu wa mkoa akamuambia boti haifai kusafiri akasema mara haiwezi kusafiri imeharibika.

“Nikazungumza na Mwakyembe akapeleka mafundi wakatengeneza, safari haikuwa rahisi, lakini changamoto zilikuwa nyingi sana, kwingine Lupingu kule ni gari moja tu ndio inayoshuka chini hakuna kupishana magari nikaambiwa nisiende nikasema nina kwenda,” alisema na kuongeza kuwa kulikuwa na ubishi mwingi wakati mwingine alionekana mtu mmoja kidogo ambaye hasikilizi ushauri sana.

Pia nyingine zinazotokana na changamoto za wananchi kutolipwa mazao yao kwa wakati, mbolea kutofika kwa wakati, halmashauri kutopata fedha za maendeleo kwa wakati, watumishi wa umma wanaohamishwa kwenda vijijini hawaendi vijijini kwenda kuwahudumia wananchi, tatizo kubwa la migogoro kati ya wakulima na wafugaji kati ya wananchi na hifadhi za taifa.

“Ndio maana mnaniona siku hizi nimenyamaza kwa sababu yale yote niliyokuwa nikiyaombea yanafanyika, umangimeza haupo watu wachape kazi wawahudumie wananchi, uadilifu unapigwa vita, rushwa inapigwa vita, uwajibikaji na uadilifu unahimizwa, utendaji kazi unatakiwa na hayo yasipofanyika mtu anaondolewa mara moja,” alifafanua Kinana ambaye kuanzia mwaka 2014 hadi mwanzoni mwa mwaka jana alitembea kote nchini akikisafisha chama chake na kuibana serikali.

Kurejea kwake CCM
“Yalitokea mazingira ambayo niliombwa na viongozi wastaafu na viongozi wa chama kuniomba niwe mtendaji mkuu wa chama chetu. Si nafasi ambayo niliipenda, bali niliitwa na nikakalishwa wakanisihi na mimi nikakubali sababu ni wito na kwa kuwa ni watu ninaowaheshimu na wana dhamana kubwa kwenye nchi yetu, nikakubali kufanya kazi hiyo,” alisema Kinana akizungumzia jinsi alivyoteuliwa kushika nafasi hiyo.

Alisema amekuwepo katika uongozi ndani ya chama kwa muda mrefu (miaka 25) ndani ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa, na alihisi ni wakati muafaka wa kung’atuka.

“Mwanasiasa mzuri ni yule anayejua wakati wa kuingia na wakati wa kutoka. Ni wakati mzuri wa kung’atuka kuachia waingie wenye umri wa kati na umri wa vijana kuachia waongoze chama na kuwaamini,”alieleza.

Alisema moja ya mambo ambayo walikubaliana wakati ule akajitahidi kukiimarisha chama, kusimamia na kumsaidia mwenyekiti kusimamia mchakato wa kuwapata wagombea kwenye nafasi zote za Urais, Ubunge na Udiwani. Pia alijitahidi kuendesha shughuli za kampeni na uchaguzi na utakamalizika.

“Uchaguzi umekwisha niruhusiwe kupumzika, na wote waliafiki na kukubali sasa muda umefika kwa hiyo nimewakumbusha yale tuliyokubaliana muda wake umefika sasa wengine wakaniuliza hivi ndivyo tulivyokubaliana nikawaambia wazee hamjawa wazee kiasi cha kusahau ndio haya tuliyokubaliana,” alieleza.

Akiombwa na JPM
Alipoulizwa kama akiombwa na Rais Magufuli aendelee kwa Katibu Mkuu, Kinana alisema, “Niseme hajasema, hatujazungumza hilo, likitokea tutaangalia, tutakaa naye kikao kama akiniomba, tutakuwa na kikao na mazungumzo muda utakapofika kama nilivyokuwa na mazungumzo na kikao kama kwa wale walioniomba mwaka 2012.”

Waliokisaliti chama
Akizungumzia walioisaliti CCM katika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, mtendaji huyo wa CCM alisema msaliti yeyote adhabu yake ni mbaya sana, hata kwenye chama cha siasa.

“Kwenye CCM wapo watu walioyumba, kulikuwa na wimbi kubwa mwaka jana, watu waliyumba hivi kidogo wakakaa mguu upande huku hawapo na kule hawapo, wako ambao sio tu waliyumba, bali walikiuka maadili na hawakushiriki kwenye shughuli za kampeni,” alisema.

Pia alisema wapo ambao hawakushiriki, hawakusaidia na wakasaidia upinzani na kila mtu atakuwa na adhabu yake kulingana na makosa yake.

“Kama mmekuwa mkifuatilia kuna waliochukuliwa hatua ngazi za wilaya na mikoa. Kwa mfano, Shinyanga 123 walichukuliwa hatua. Wapo wanaotakiwa kuchukuliwa hatua kwenye ngazi za juu, sasa jambo moja mtu yeyote kabla ya kuchukuliwa hatua lazima aelezwe mashtaka yake, apewe fursa ya kusikilizwa, kwa hiyo hawa wote watasomewa mashtaka, watasikiliza na kupewa adhabu kwa kadri itakavyostahili, lakini hatua zitachukuliwa mara baada ya Mkutano Mkuu kumalizika,”alieleza.