Sunday, January 20, 2019

Mwezi mkubwa mwekundu kuonekana duniani


Mwezi mkubwa mwekundu
Watu kote duniani wanatarajiwa kuona kupatwa kwa mwezi utakaobadilika na kuwa mwekundu .
Wakati wa kupatwa kwa mwez,i dunia hutoa kivuli chekundu.
Kupatwa huko kwa mwezi kutaonekana kutoka kaskazini na Kusini mwa Marekani pamoja na maeneo ya magharibi mwa Ulaya ikiwemo Uingereza na kaskazini mwa Afrika

Kupatwa kwa mwezi ni nini?

Tukio hili hujiri wakati dunia inapopita katikati ya Jua na mwezi.
Katika hali hii, jua huwa nyuma ya dunia huku mwezi ukizunguka katika kivuli cha dunia.

Je mwezi mwekundu ni upi?

Maelzo ya mwezi mwekundu
Presentational white space

Je mwezi huo utakuwa mwekundu?

Ndio. Baadhi ya watangazaji huuita "super blood wolf moon".
Jina "super" linatokana na ukweli kwamba mwezi huo utakuwa karibu sana na dunia ambapo utaonekana kuwa mkubwa angani zaidi ya kawaida.
Nalo Jina "wolf" linatokana na majina yanayopewa miezi mikubwa mwezi Januari "wolf moons".
Walter freeman , naibu profesa katika chuo kikuu cha Syracuse University mjini New York state, alisema: "mwanga mdogo wa jua hutolewa na dunia na kufika katika mwezi, ukijipinda kando kando ya dunia.
Kiwango hiki cha rangi nyekundu huangazia mwezi vya kutosha kwa binadamu kuweza kuona.

Wapi na lini nitauona mnwezi huo?

Kupatwa kwa mwezi kutaanza mwendo wa 02:35 GMT siku ya Monday na kukamilika katika saa 07:49 GMT, lakini kipindi ambacho mwezi wote utakuwa mwekundu kitakuwa mwendo wa 05:12 GMT.
Nchini Uingereza mwezi utakuwa juu ya upeo wa macho katika kipindi chote cha kupatwa kwa mwezi ijapokuwa kusini mashariki mwa Uingereza, jua litaonekana kupaa huku luna hiyo ikikamilika.
Kupatwa huko kutaonekana kaskazini magharibi mwa Ufaransa, kaskani magharibi mwa Uhispania, Ureno, na eneo dogo la Afrika magharibi, karibu eneo lote la kaskazni na Amerika Kusini, mashariki mwa Pacific pamoja na kilele cha Ksakzini mashairiki mwa Urusi.

Je ni salama kuutazama?

Huku matukio ya kupatwa kwa mwezi yakitajwa kuwa hatari kutazama moja kwa moja, mwangaza wa kupatwa kwa mwezi ni mdogo hivyobasi ni salama kutazama bila kutumia vifaa vyovyote.

Je ina muhimu gani?

Tukio hilo ni la mwisho kwa watazamaji wa anga nchini Uingereza kuona kupatwa kwa mwezi kwa kipindi cha muda mrefu hadi 2029- hali ya hewa itakaporuhusu.